Sauti za Ziwani: Uchambuzi wa Nyimbo za Uvuvi za Kisukuma kama Chombo cha Mawasiliano ya Jamii katika Mwambao wa Ziwa Victoria

Authors

  • Steven Yesaya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino, Tanzania Author

DOI:

https://doi.org/10.33687/ijef.003.03.00141

Keywords:

Nyimbo za uvuvi, Wasukuma, mawasiliano ya jamii, fasihi simulizi, Nadharia ya Uamilifu

Abstract

Makala hii inachunguza mchango wa nyimbo za uvuvi za Kisukuma kama chombo cha mawasiliano ya jamii na maendeleo ya kijamii miongoni mwa wavuvi wa mwambao wa Ziwa Victoria. Utafiti umeongozwa na Nadharia ya Uamilifu iliyoasisiwa na Bronislaw Malinowski, A.R. Radcliffe-Brown na Franz Boas. Data zilikusanywa kupitia usaili na ushuhudiaji shirikishi miongoni mwa wavuvi wa jamii ya Wasukuma katika Mkoa wa Mwanza. Matokeo yanaonesha kuwa nyimbo za uvuvi hutumika kuhamasisha uwajibikaji, kuimarisha mshikamano, kueleza hisia mbalimbali na kutoa tahadhari kuhusu hatari zinazoweza kujitokeza ziwani. Aidha, nyimbo hizi huchangia katika kuhifadhi maarifa ya jadi na kuendeleza maadili ya kazi. Makala inahitimisha kuwa nyimbo za uvuvi za Kisukuma ni zaidi ya burudani; ni nyenzo muhimu ya mawasiliano na urithi wa kitamaduni unaostahili kuhifadhiwa na kuendelezwa.

Downloads

Published

2026-07-21

Issue

Section

Research Articles

How to Cite

Sauti za Ziwani: Uchambuzi wa Nyimbo za Uvuvi za Kisukuma kama Chombo cha Mawasiliano ya Jamii katika Mwambao wa Ziwa Victoria (S. Yesaya , Trans.). (2026). International Journal of Education Foundations, 3(3), 555-563. https://doi.org/10.33687/ijef.003.03.00141

Similar Articles

11-20 of 99

You may also start an advanced similarity search for this article.